Alhamisi februari 18
Tulikaa kwa Joshua, mji uliokua masaa matatu kutoka Nairobi. Mipango ilibadilika kidogo na ikabidi ni shughulike kujulisha serikali juu ya shughuli zangu za hapo kambiti.
Ilinikumbusha Sweden vile mtu akitaka huduma anazungushwa kutoka mahali moja hadi nyingine. Ni vile hatutaki kusghulikia jamii.
Tuliamua kufika Kambiti leo badala ya jana. Usiku ulijaa mvinyo, chakula na vicheko tukisherehekea mwanzo wa mradi wetu.

Tulikuja kwa njia ilio na shimo nyingi. Lakini mazingira yalikua mazuri sana. Kulikua na furaha tele nilipoonana na Joshua na Julius. Mwisho kuwaona ni kama mwaka moja uliopita. Sasa tumepata kuonana tena. Kulikua na mbuzi wengi, ng'ombe, na kuku. Tuliweza kusikia mbwa ikibweka huko nje na tukaona paka zikizurura kila mahali. Kulikua hakuna stima, maji wala joto. Nilijiuliza ni vipi wanaishi wakati wa baridi. Choo ni tofauti kabisa na ile ya nyumbani mwangu. Ni choo cha shimo na shimo yenyewe ni ndogo zaidi hadi nikashtuka vipi nitakavyoitumia.
Leo tulishinda na Joshua na Julius na familia zao tukizunguka mtaa wao. Tulitrekodi kidogo na tukafanya mkutano mdogo alafu tukalala.

KUHUSU KAMBITI: NI kijiji katika eneo la wamunyu, nyumbani mwa kabila ya wakamba. Huku kuna misitu, na milima mengi. Boma la wakamba huwa na nyumba kadhaa za mawe ama tofali na paa huwa mabati. Nyumba nyingi hazina maji wala stima. Watu wa huku huongea kikamba, lakini waliobahatika kuenda shule huongea pia Kiswahili na kiingereza.
Write a comment