Jumapili, Februari 14

Mda unazidi kuyoyoma, na kila siku mambo mapya yanajitokeza. Ndio maan nina hisi kama nimeishi Kenya miezi mingi. Kila siku majaribio ni mengi. Leo ni jumaili na kama kwaida ni siku ya kuenda kanisisani. Majirani wangu wamejivalia nguo zao za kupendeza. Saa nne kamili inatupata tumekaa katika kanisa ambayo Joshua na Julius huenda. Baada ya nyimbo kadhaa, michezo ya kuigiza na dansi, mhubiri alianza kuhuburi neno. Alisema maneno mazuri na jinsi alivyokua anaongea ilisisimua watu. Lakini kanisa yenyewe haikua vyema. Masikio yangu ilijaribu kubainisha kati ya maneno na kelele. Mimi ni mtu anayehangaika sana, na katika hali kama hiyo nachoka kwa urahisi na nahisi kuwa mgonjwa. Na kuongeza chumvi kwa kidonda, mhubiri alionge kwa Kiswahili, lugha nisichokielewa. Ilibidi nivumilie sana nisilie kwa mahangaiko. Winston alijaribu kwa uwezo wake kunipiga picha lakini hata yeye alikua anahangiaka. Baada ya masaa mawili Winston aliniuliza, " Kwani Kanisa hii haikwishi?". Ilikua tayri ni saa saba mchana. Namgeukia Joshua nikijaribu kadri ya uwezo wangu nisilie nikamuuliza "kanisa yaisha saa ngapi?" akanijibu " saa kumi". Nilimweleza Winston na hakuamini masikio yake. Hatangeweza kufanya lolote na kwa hivyo tuka kaa na kusikiza. Baada ya masaa mangine matatu kanisa ilikwisha na nikajihisi mshupavu wa kuvumilia yaote hayo.


Mahojiano ya Jana yalitupa uchovu mwingi sana. Tulijaribu kutafuta takwimu ya kuvutia kuhusu maisha ya mhusika mmoja katika filamu yetu. Lakini pia, isingekuwa vyema kujihususha sana na maisha ya mhusika huyo kwasababu hatukua na uwezo wa kumsaidia. Hii ndio changamoto ambayo tunapambana nayo kila siku.

Write a comment