IJUMAA FEBRUARI 26
Jana niliamka nikihisi ugonjwa. Nilijaribu kuamka lakini nikalemewa nikarudi kitandani. Nilikua na shida ya tumbo. Baada ya masaa ya uchungu na kutapika, nikaamua niende hospitalini. Daktari alinipa madawa na nikarudi hotelini. Lakini nikaanza kupata jot ya mwili.
Siku ya leo ndio siku ilikua na joto zaidi, nyuzi 35 kwa kivuli. Bado sikujihisi mzima, lakini ilibidi kazi iendelee. Nilikua na furaha maanake nilikua nimenunua vitu nitahitaji nikiingia kwa nyumba yangu ya Kiswahili. Nitahamia huko kesho.

Nyumba yangu ya Kiswahili ni ndogo na ina wadudu, nzi na mbu. Itakua ngumu kuishi hapo. Kuelewa vizuri maisha yangu hapo lazma uone filamu yangu.
Huko Sweden watu wanajitayarisha kuenda kustarehe kwa vilabu na marafiki lakini hapa Kenya lazma tuchape kazi siku zote saba za wiki.

Write a comment