November 2010

JUMATATU FEBRUARI 22


Changamoto kuu tulilolipata katika mji wa Wamunyu ni ukosefu wa nguvu za umeme. Kamera yetu ilihitaji moto. Ilibidi tutafute jenereta ili kuitia moto kamera yetu.
Katika mji huo kulikua na soko. Mkulimia mmoja aliku amesimama na mbuzi na ng'ombe zake. Tulipata mahali pakuweka mitambo yetu alafu tukazuru mji huo. Watu walituangalia sana, wengine wakituita "MZUNGU" na wengine wakisema ‘MAMBO'.


Mara tukasikia mtu akipiga kelele akisema "MWAMERICA, wewe MWAMERICA". Mtu mlevi alitukujia akiyumba yumba. Akasimama na kutupa mkono wake to msalimie "Habari wamerica, karibuni wamunyu". Tulishangazwa sana lakini tukamsalimia hata hivyo. Tuliongea na yeye kidogo alafu tukaendelea kutembea.
Mwanamme huyo alitufuata kila mahali tulipoenda. Tulijaribu sana kumfukuza, na kumtoroka lakini alikua yuatupata tu. Bado aliku anatuita wamerica na akaanza kubadili nia yake kwetu. Alianza kutuita na ukali. Mwishoe alinikaribia kwa maskio na kusema " wewe mwanaume, Bwana America. Naongea na wewe". Tulipoteza hisia za usalama wakati huo.
Joshua aliku upande mwengine mwa bara bara. Alikua anacheza bao na marafiki zake. Rose alijaribu kumwambia mwanamme huyo awachane nasi lakini akamjibu Rose "Siongei na wewe, naongea na Bwana America." Kitu cha kuchekesha ni kwamba alikua na bendera ndogo ya America ambayo alianza kupepea akisema "Ameeeriiican, Ameeerrriccan!"
Joshua alitokea na akaongea na mtu huyo alafu akaondoka. Nilimwangalia Joshua nikijiuliza nini alichomwambia ndio mtu huyo ili aondoke.
Siku chache baada ya leo tutasafiri kuenda Mombasa ambapo Joshua hufanya kazi. Ni safari ambayo hufanya mara moja kwa mwaka.



Jumatatu Februari 22


Mada ya leo imehusu choo. Imekua shida kuenda haja kubwa, ktu ambacho sijatilia maanani huko nyumbani Sweden. Huko Sweden ni lazma tuanze keshimu choo. Baada ya siku nyingi, na mahojiano mengi Winston alitueleza tujaribu kuona choo hicho kama choo cha hoteli alafu tutaweza kuitumia.



Lakini kwa sasa ilibidi tupakie mitambo yetu na tuende jijini. Tukiwa njiani, nilihisi kuenda haja kubwa. Tulitafuta choo kwa muda lakini tukapata choo moja kando ya duka la fundi wa simu. Choo hicho kilikua kichafu kupindukia. Nilijaribu kuingia, lakini nikifika ndani nalemewa na harufu mpaka inanibidi nitoke. Nilianza kulia na Winston akaanza kunicheka.
Tukirudi nyumbani kwa Joshua, tulipanga na Annette vile ataenda kutumia choo cha Joshua. Baada ya kula chakula cha jioni cha maharagwe, Annette alilazimika kutumia choo. Akajiamii na taa na manukato na akaenda chooni. Shida ya harufu ilitatuliwa.



Kesho kutakua na shughuli nyingi. Lazima tuamke mapema kupiga filamu ya jua ikipaa, halafu niwatengenezee watoto chai ili waende shule. Alafu tutaona mbuzi akichinjwa.

JUMAPILI FEBRUARI 21


Leo imekua siku iliyozaa matunda mengi. Siku ambayo najihisi nimfanya kazi ya maana.
Asubuhi, tuliskiza hadithi ya Joshua kuhusu maisha yake ya utotoni.Hadithi ambayo ilikua tofauti na yangu ya Iran ama ya Winston ya New Zealand. Hadithi ya ukweli. Tulirekodi filamu kila mahali tulienda. Saa zingine tulichanganyikwa na kitu cha kuweka filamu maanake mabo yalikua mengi. Ilibidi tuchukue kila kitu maanake wakati mwingine vitu vidogo vidogo ndivyo hufanya filamu ikawa nzuri. Tulipanda piki mbili, watatu kwa kila moja, na kuenda kwa nyumba ya Julia ambayo ilikua kilomita 3 hivi na nyumba ya Joshua. Kukutana na Julia ilinifanya nione kwamba hata kama hawana mali nyingi, wamejaa na furaha na tabasamu kwa maisha yao.



Tuliongea na mamake Julia ambaye alitupa hisia na maoni yake mengi. Mwanamke wa miaka 90 na aliye na nguvu na furaha. Hadithi zake zilikua za kusisimua. Alikua mwanamke mwenye roho safi. Nahisi kama tumeendelea sana kama dunia lakini tumepoteza uanadamu wetu na badala yake ni chuki, tama, uwivu na mengineyo.



Nilipongea na bibi ya Julius nilipata kujua megi kuhusu maisha yao. Wamekua wakiishi kama bwana na bibi kwa miaka 13. Katika miaka hiyo yote wameshindwa kupata motto. Kwa Mary kupata motto itabidi atumie pesa nyingi na apate madawa mengi. Na pesa hiyo aliku hana kabsa.
Julius alitukaribisha chai kwa mkahawa moja. Baada ya chai tulipanda piki piki na kurudi nyumbani kwa Joshua. Jioni tukapika chakula cha join na bibi ya Joshua.


Sijui kwanini lakini huku kambiti nahisi njaa kila wakati. Labda ni kwasababu nala kiamsha kinywa na chakula cha join pekee yake.

JUMAMOSI 20 FEBRUARI


Ilikua saa tatu za usiku. Tulilala mahala padogo, mwili wangu umeegezwa kwa ukuta ndio tutoshee kwa kitanda. Tuliongea juu ya siku yetu huku tukiskia milio ya popo wakiwa nje. Baada ya mda mchache nilihisi kuenda choo ambayo ilikua nje. Wenzangu walisema watiniunga.
Nje kulikua na giza totoro, hukuweza kuona hata pua chako. Mara tukasikia kelele kwa shamba ilio kando na hapo. Tulijua kwamba sisi ndio pekee tulio macho, huyu kwani ni nani? Haja ya kunipeleka choo ilipotea, huku nikishikilia tochi lisilokua na mwangaza tosha nilijaribu kubainisha ni nani aliyekua anatembea shambani wakati huu. Tulitulia tuli, mbwa iliyo karibu nanyumba yetu ilianza kubweka. Uoga ukatuzidi, tukaanza kutafuta njia ya kurudi kwa chumba chetu. Winston na Annette walikua nyuma yangu. Tulburutana kwa kasi tukijikwaa ili tufike haraka. Mwishoe tulifika salama, tukaingia ndani na kufunga mlango na kifuli alafu tukaweka mabagi zetu kuzuia mlango zaidi. Moyo wangu ulikua unapiga haraka huku nikijaribu kusikiza nje kuna nini. Baada ya mda mfupi tukasikia mtu nje na uoga ukazidi.



Wakati ulipita, nikitazama nje. Moyo bado wanidunda kwa uoga. Sikua najihisi niko salama, nikashinda nikiamsha Winston kujua kama amelala. Usiku huo sikupata hata lepe la usingizi.